Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, August 6, 2011

HAPA NA PALE KUTOKA MKOANI MBEYA

SHILINGI MIL 52 ZIMETOLEWA KUTUMIKA KIPINDI CHOTE CHA MAONESHO YA NANENANE MKOANI MBEYA

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana John Livingstone Mwakipesile

Zaidi ya shilingi milioni 52 zimetolewa kutumika katika kipindi chote cha maonesho ya kilimo Nanenane yanayoendelea kwenye uwanja wa John Mwakangale jijini Mbeya.

Akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa mkoa wa Mbeya John Mwakipesile amesema fedha hizo ni kwaajili ya shughuli za maonesho ili yafanywe na ya vutie miongoni mwajamii.

Aidha ameitaka kamati ya kusimamia maonyesho hayo kuakikisha fedha zilizopatikana zinatumika kama ilivyo kusudiwa na kuwataka wamiliki wa wa vibanda vilivyopo nje ya uwanja huo kuvikamilisha ili kuondokana na hatari ya kufutiwa usajili wa maeneo yao.

WALEMAVU WAVVU NCHINI TANZANIA WASHAURIWA WASIKATE TAMAA
Watu wenye ulemavu na wale wanaoishi na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi wameshauriwa kutokata tamaa ya maisha pindi wanapakabiliana na changamtoto mbalimbali ndani ya jamii.

Ushauri huo umetolewa na mkuu wa kikundi cha jipe moyo bwana Kaspery Ngairo wakati wa mahojiano kuhusu mpango walionao kuwawezesha watu wenye ulemavu na wale wanaoishi na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi

Amesema watu wenye ulemavu wanamchango mkubwa katika kukuza na kuendeleza shughuli za kimaendelea hapa nchini nakwamba jamii inatakiwa kuondokana na dhana ya kuwa walemavu hawana mchango katika kukuza na kuleta maendeleo ya Taifa.

Aidha Ngairo ameiomba jamii kuondokana na dhana ya kuwa ukimwi una ambukizwa kwa kula ama kuzungumza na mtu mwenye maambukizi hayo na badala yake amewataka kutambua kuwa mtu unaweza kupata maambukizi ya Virusi vya ukimwi kwa kuchangia nyembe, Ngono zembe, kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na Uchangiaji wa damu isiyo salama.

WILAYA YA KILOLO MKOANI IRINGA YAONGEZA UZALISHAJI WA MAZAO MWAKA HUU.
Halmashauri ya wilaya ya Kilolo mkoani Iringa imeongeza uzalishaji wa mazao mwaka huu kutokana na wakulima kutumia mbegu bora pamoja na kilimo cha umwagiliaji.

Hayo yamesemwa na Afisa kilimo wa wilaya hiyo Bwana Logan Moses katika maonesho ya kilimo Nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.

Amesema kuwa zao la mahindi limepanda kutoka tani elfu 82 hadi kufikia tani elfu 91 na vitunguu kutoka tani elfu 80 hadi kufikia tani laki moja huku nyanya imepanda kutoka tani laki moja na thelathini na moja hadi kufikia tani laki moja na sitini na tano.

Aidha amewataka wananchi hususani vijana kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuongeza nguvu katika kilimo ili kuleta maendeleo kwa jamii na taifa kwa ujumla.

BEI YA MAHINDI YASHUKA KWA ASILIMIA 3 WILAYANI MOMBA MKOANI MBEYA.
Bei ya gunia la mahindi imeshuka kutoka shilingi elfu 31 hadi kufikia elfu 28 wakati debe la maharage kushuka kutoka elfu 22 hadi shilingi elfu 18 katika wilaya ya Momba mkoani Mbeya.

Wafanyabiashara na wakulima wa wilayani hiyo wamesema kushuka kwa bei ya mazao kunatokana na kuwepo kwa mavuno mengi .

Mmoja wa wakulima hao Bwana Elius Kaminyoge amesema pamoja na kushuka kwa mahindi na maharage katika soko la majengo pia zao la ulezi limeshuka kutoka shilingio elfu 43 hadi kufikia shilingi elfu 41 kwa gunia na vitunguu kushuka toka shilingi elfu 25 hadi kufikia elfu 18 kwa debe.

Amesema sababu ya kushuka kwa bei ya mazao hayo kunatokana na wakulima kuingiza mazao kwa wingi sokoni hapo.

No comments: