Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, July 12, 2011

MWAKALELI SEKONDARI SI SHWARI

WAziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Dkt Shukru
Habari zilizoufikia mtandao huu hivi mchana huu kutoka Tukuyu mkoani Mbeya zinadai kuwa hali si shwari katika shule ya sekondari Mwakaleli iliyopo mkoani humo baada ya wazazi na wanafunzi kuanza fujo kupinga watoto wao zaidi ya 20 kufukuzwa shule.

Imedaiwa kuwa wazazi hao walifika shuleni hapo kuitika wito wa bodi ya shule hiyo baada ya watoto wao kudaiwa kuonyesha utovu wa nidham na kusimamishwa kwa muda kabla ya leo kutakiwa kufika shuleni hapo ili kusikiliza madai ya viongozi wa shule hiyo dhidi ya wanafunzi hao ila haikuwa hivyo baada ya bodi ya shule kuonyesha kutofautiana na wazazi na wanafunzi hao baada ya kutaka baadhi ya wanafunzi kufukuzwa kabisa shule .

Hadi sasa jeshi la polisi limeanza kusogea eneo la shule hiyo ili kutuliza ghasia zaidi .
undani wa sakata hili utaupata mara baada ya mwandishi wa mtandao huu kufika eneo la tukio

Habari kwa hisani ya Fransic Godwin

No comments: