Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, September 18, 2012

BAADA YA NIGERIA SASA MBEYA: MWANAMKE AJIFUNGUA KIUMBE KINACHOFANANA NA NG'OMBE


*Kichwa cha ng'ombe.
*Kiwiliwili cha binadamu.

Na Ezekiel Kamanga,Chunya.
Mwanamke mmoja ambaye amefahamika kwa jina la Shija Paulo(35),mkazi wa Kijiji cha Magaga,Kata ya Mbuyuni Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya amejifungua kiumbe kinachofanana na ng'ombe chenye jinsi ya kiume.

Tukio hilo limetokea Septemba 16 mwaka huu majira ya saa 11 alfajiri,mwanamke huyo alipokuwa amepelekwa katika Zahanati ya Mbuyuni kwa ajili ya kujifungua akiwa na mumewake Bwana Mwigulu Yangula(Makeni) lakini kabla ya kufika zahanati mwanamke huyo alipatwa na uchungu ndipo alipoomba msaada kwa Mkunga wa jadi aliyekuwa karibu Bi. Agripina Fredrick Sikanyika(Namwinje).

Mkunga huyo alimpokea mwanamke huyo na kujifungua salama huku kiumbe hicho kikiwa na kichwa na domo mithili ya ndama(mtoto wa ng'ombe) chenye dalili ya kuota mapembe na manyoya meusi hadi eneo la kifuani ambapo kutoka hapo kifuani mpaka miguuni alikuwa na umbile la binadamu na jinsi ya kiume  licha ya kutimiza miezi tisha ya kuzaliwa na uzito wa wastani.

Hali hiyo ilimtisha sana Mkunga Bi. Sikanyika na kuitwa Bwana Yangula kushuhudia kiumbe hicho naye alistaajabu kwa yale yaliyotokea.

Hata hivyo kiumbe hicho kilidumu kwa muda wa masaa  matatu na kufariki dunia na katika uchunguzi wa mwandishi wa habari hii amebaini kuwa hiyo ilikuwa ni mimba ya nane kwa mwanamke huyo na kila mimba hupata watoto ambao si riziki.

Tukio hilo pia lilishuhudiwa na mhudumu wa Kituo cha Afya,kitongoji cha Magaga Bwana Josephat Alisen Ismail,ambaye naye amesema ameshangazwa na tukio hilo na kusema hajawahi kukutana na jambo hilo katika taaluma hiyo ya utabibu.

Wakati wa tukio hilo Afisa Mtendaji wa Kijiji Bwana Michael Sanziwa hakuwepo na alipopigiwa simu aliruhusu kiumbe hicho kichukuliwe na mzazi ambapo maziko yake yalifanyika kandokando ya nyumba ya Bwana Yangula.

Katika tukio hilo watu wengine wamelihusisha na imani za kishirikina na wataalamu wa viumbe wamesema kuwa mara nyingi viumbe hivyo huwa haviishi muda mrefu,lakini hali ya mama aliyejifungua inaendelea vema baada ya kujifungua.

No comments: