Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Sunday, July 31, 2011

KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA IRINGA YAPATA VIONGOZI WAPYA FRANCIS GODWIN AULA UKATIBU MSAIDIZI


Baadhi ya wanachama wa IPC wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waliochaguliwa kuongoza IPC ,mwenye pama katikati ni mmiliki wa mtandao huu Bw Francis Godwin ambaye alipita bila kupingwa katika nafasi ya ukatibu msaidizi wa IPC

Katika uchaguzi huu viongozi walioanguka katika uchaguzi huo ambao walikuwemo katika safu ya uongozi katika uongozi uliopita ni pamoja na Sima Bingileki ambaye alikuwa makamu mwenyekiti,huku Eliasa Ally ambaye alikuwa mjumbe kipindi kilichopita akijitoa kugombea tena nafasi hiyo na Kenneth Simbaya akiamua kustaafu nafasi ya kiti pamoja na Hakimu Mwafongo ambaye hakugombea tena nafasi ya ukatibu msaidizi .

Katiba nafasi ya uweka hazina msaidizi Vicky Macha wa Nipashe Iringa alipita bila kupingwa huku nafasi ya katibu msaidizi pia Francis Godwin mwandishi wa gazeti la Tanzania daima Irina ,kurugenzi wa kampuni ya Free Community Media's na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari za jinsia Tanzania (TGNP) mikoa ya kusini akipita bila kupingwa pamoja na wajumbe 13 7 wa kamati ya utendaji ndani ya IPC pia wakipita bila kupingwa kufuatia Eliasa Ally kujitoa katika kinyang'anyiro hicho.

Wajumbe 13 wanaounda kamati ya utendaji ndani ya IPC ni pamoja na Daud Mwangosi, Frank Leonard ,Zulfa Shomary, Francis Godwin, Suleman Boki,Vicky Macha, Getrude Madembwe, Shabani Lupimo, Frederick Siwale,Conard Mpila,Fulgence Malangalila,Janeth Matondo na Jackson Manga .

PICHA  ZAIDI INGIA HAPA

No comments: