Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, August 23, 2012

WANAMKE AJIFUNGUA KICHANGA NA KUKIZIKA


Habari na Ezekiel Kamanga,Chunya.
Mwanamke mmoja Bi. Tabu Elias mkazi wa Kitongoji Nambalwe Shina la Mwilonga,Kata ya Magamba,Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya,amejifungua mtoto wa kike na kumzika muda mfupi baada ya kujifungua.

Tukio hilo limetokea Agosti 22 mwaka huu kijijini hapo majira ya saa 11:30 jioni,ambapo mwanakme huyo alimzika mtoto huyo chumbani katika nyumba anayoishi.

Bi Tabu ametenda ukatili huo wakati mumewe Bwana Gilbert Nzowa,alipokuwa kazini na ndipo aliporejea majira ya saa 12 jioni alimkuta mkewe akiwa hana ujauzito na kumuuliza mkewe kulikoni,ndipo alipomueleza kuwa amejifungua mtoto wa kike na kumzika.

Taarifa hiyo ilimkasirisha Bwana Gilbert na kuchukua jukumu la kutoa taarifa kwa Katibu wa Shina Bwana Juma Chakupewa Chapotea Mwabulambo ambapo aliongozana hadi eneo la tukio ambapo mwanamke huyo alikiri kutenda kosa hilo.

Aidha Katibu huyo aliamuru Bi Tabu kufukua shimo ambalo alimzika mtoto huyo na kulitekeleza agizo hilo ambapo baada ya kumaliza kufukua alikutwa mtoto huyo akiwa amevalishwa nguo mpya na tayari akiwa ameshafariki.

Baada ya kupatikana mtoto huyo,alipoulizwa kwanini ametenda kitendo hicho,mwanamke huyo alidai tumbo lake lilikuwa likimuuma kwa muda mrefu na hata alipojifungua hakufahamu kama kajifungua mtoto hai na ndipo alipoamua kumzika mumewe akiwa hayupo.

Bwana Mwabulambo alimchukua mwanamke huyo mpaka Ofisi ya Kitongoji na kisha kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa kitongoji hicho Bwana Mapinduzi Kailote.

Kwa upande wake Bwana Kailote alisema suala hilo ni gumu kwake kwa hiyo haitakuwa rahisi kutolea maamuzi,ndipo walipoolekea katika Ofisi za Kijiji cha Magamba ili kupata taaribu za kutoa taarifa Kituo cha Polisi Galula.

Hata hivyo hivi karibuni inadaiwa kuwa Bi Tabu Elias alionekana kama mwenye matatizo ya akili.

No comments: