Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, September 17, 2011

GARI LA MBUNGE MKOANI MBEYA LAPATA PANCHA WAKATI AKIELEKEA KUOKOA JAMII

Waandishi wa habari wakisaidia kumsaidia Mbunge wa Viti maalum Dk Mary Mwanjelwa kufungua taili la lilolopata Pancha wakati akienda kutoa msaada wa Magodoro 60 katika hospitali ya Wilaya ya Itumba - Ileje, ambayo ni kwa ajili ya matumizi ya chumba cha wazazi na watoto. (Kushoto ni Solomon Mwansele wa Uhuru na Joachim Nyambi wa Habari leo)
Dk Mwanjelwa akiwasili katika katika Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Ileje Bi Ester Wakari.
Mkuu wa wilaya ya Ileje Bi Ester Wakari akijiandaa kupokea ugeni wa baraka.
Dk Mwanjelwa akisalimiana na Katibu wa Umoja wa wanawake wilaya ya Ileje
Magodoro ambayo yametolewa na msaada wa Mbunge wa viti maalum Dk Mwanjelwa katika Hospitali ya Wilaya Itumba Ileje.
Dk Mwanjelwa akikumbatiana na baadhi ya Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM baada ya kutembelea Ofisi za Chama hicho Wilaya.
Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Ileje Bwana Aliko Kibona akimkaribisha Mbunge wa viti Maalum Dk Mary Mwanjelwa, katika ofisi yake.
Daktari wa Hospitali ya Wilaya ya Ileje Ronatus Kilolo akimuongoza Dk Mwanjelwa kukagua Vitengo vya huduma mbalimbali zitolewazo na Hospitali yake.
Wabunge wakimfurahia mtoto aliyezaliwa siku ya jana katika ziara yao hospitalini hapo na kubaini kuwa kkunaupungufu wa vitanda vya Kujifungulia akina Mama wajawazito.
Wageni na wenyeji wakiongozana na Dk Mwanjelwa na kutembelea maeneo mbalimbali ya hospitali hiyo
Mganga mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Ileje Ronatus akipogea magodoro 60 yaliyotolewa kwa msaada na Mbunge Vitimaalum Dk Mwanjelwa.
Dk Mwanjelwa akivishwa Skafu kukaribishwa katika Mahafali ya Kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Ndola Ileje.
Dk Mwanjelwa akiwahutubia wa hitimu wa kidato cha nne na kuwaasa kuzingatia elimu na kuaidi kuipa shule hiyo ya Sekondari vitabu Maboksi mawili.
Mbunge Vitimaalum Dk Mwanjelwa akiwa katika picha moja na wahitimu wa Kidato cha nne katika shule ya sekondari Ndola Ileje.

1 comment:

Anonymous said...

ASANTE KWA MBUNGE KWA MSAADA WA MAGODORO.HONGERA KIDATO CHA NNE NDOLA NA ILEJE KWA UJUMLA,MKAJITAIDI KATIKA PEPA.MUNGU AWABARIKI SANA,,,JAH LIVE.RAS ERICK