Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, April 11, 2011

HUDUMA YA NABII JOSHUA YAZIDI KUVUTA WATU WILAYANI MBOZI

 Baada ya kupata matone ya maji mama huyu ambaye alifika na mkongoja wake kwaajili ya kumwezesha kutembea sasa ameuweka begani akitembea kumfuata nabii Joshua ambaye aliendesha uponyaji katika uwanja wa Mlowo juzi na jana.  
Nabii Joshua akitoa ujumbe juu ya Tanzania na mchakato wa katiba kutokutumika katika kuvuruga hali ya amani anaeleza kuwa maono yanamwonyesha kuna dalili za kutokea vurugu kutokana na mchakato huu wa katiba, anakemea kutotumika kwa viongozi wa dini na wanasiasa kwa maslahi yao badala yake ajenda ya mabadiliko ya katiba iendeshwe kwa kuzingatia maslahi ya taifa huku amani, utulivu na umoja vikilindwa  kwa njia ya maombi.  
NABII JOSHUA AKITOA MATONE KWA WANANCHI WALIOFIKA KUPATA HUDUMA YA KIROHO KUPITIA MATONE YA MAJI KUTOKANA NA MATATIZO YA KIMWILI, KISAIKOLOJIA NA KIUCHUMI YANAYOWAKABILI KATIKA UWANJA WA MLOWO.
Mtume Msigwa akitoa maelekezo kwa watu waliopanga foleni kujiandaa na matone yanayotolewa na  NABII JOSHUA


No comments: